Mwaka 2019 Lazima Niolewe Nimechoka Kusubiri- Tiko

Muigizaji wa Bongo movie na msanii wa Bongo fleva Tiko Hassan ameibuka na kuweka wazi nia yake kutaka kutafuta mume na kuolewa kwa mwaka huu wa 2019.

Tiko amefunguka na kusema yeye Kama mwanamke ambaye anajiamini kuwa amekamilika anatamani sana apate mwanaume wa kuwa mwenza wake kwani amechoka kusubiri.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Tiko alisema kuwa ndoa ni heshima kwa kila mwanamke na amesubiri kwa muda mrefu bila mafanikio lakini imani yake ni kwamba, atauona mwaka wa 2020 akiwa ni mke wa mtu.

Jamani nimechoka kusubiri lakini naamini mwaka huu utakuwa ni mzuri kwangu, kila kwenye ibada namuomba Mungu anijaalie mume bora ndani ya mwaka huu“.

Lakini pia Tiko ameweka waiz anataka mwanaume ambaye atakuwa na utayari wa kumuelewa kutokana na kazi anayofanya.

Tiko Awasahauri Wasanii wa Bongo Kuwa Watiifu kwa Serikali.

Msanii wa bongo movies nchini Tiko Hasssan amefunguka na kuwataka wasanii wa bongo kuwa watiifu pale wanapoambiwa kutekeleza jambo na serikali ili wasiweze kupatwa na madhara maengine yanayoweza kutokea baada ya kukiuka sheria hizo.

Tiko amesema kuwa kuna baadhi ya wasanii unakuta wanahitajika kufika mahali flani na mamalaka inayohusiana na sanaa lakini wanakiuka maagizo hayo alafu ukifika muda wa kuipoea adhabu anakuwa mkali na wa kuanza kulalamika wakati picdi wanapokuwa wanaitwa inakuwa ni kwa manufaa ya kazi zao wenyewe za sanaa .

Akitolea mfano kutoka kwa wasanii wa muziki, Tiko anasema kuwa serikali kupitia Baraza la habari, sanaa , tamaduni na michezo wamekuwa wakiwaita wasanii ili kukaaa nao chini kuzungumza nao kuhusu marekebisho ya kazi zao hasa wasanii wa muziki lakini wanakuwa wanapuuzia na kushinwa kufika kwa kudharau.

Jamani mastaa tunatakiwa kuheshimu serikali , aple unapoitwa  wito unatakiwa kutii wito huo. kwa sababu hiyo ndo inayosaidia katika kazi za sanaa.- Alifunguka Tiko Hassan alipokuwa akiongea na  za moto moto news.

Haya yote yanakuja baada ya wki moja iliyopita wasanii wengine kukumbwa na sakata la kufungiwa kwa kazi zao na serikali kwa madai ya kwenda kinyume na maadili ya Tanzania katika utoaji wa kazi zao na mavazi yao kitu ambacho kimewaumiza wasanii wengi huku baraza la sanaa likisema kuwa wasanii hao wamekuwa wakipuuzia wito na barua za mazungumzo wanazotumiwa.