Vanessa Mdee na Gabo Waunga Mkono Harakati Za BASATA

Msanii wa Bongo fleva anayefanya vyema kabisa Vanessa Mdee na Muigizaji bora wa Kiume wa Bongo movie Gabo Zigamba wameonekana kuunga mkono harakati za Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA).

Wiki iliyopita BASATA ilitangaza sheria mpya kwa wasanii wote Tanzania kuwa wanaenda kujisajili BASATA mara tu wanaenda Safari za nje ya nchi Kwenye shoo mbali mbali.

Vanessa Mdee na Gabo wameonekana kuwa mstari wa mbele kuinga mkono na kutoonekana sheria hiyo kwani wameenda kuomba kibali kw ajili ya kusafiri nje ya nchi kwa kazi zao za sanaa.

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Kaimu Katibu Mtendaji wa BASATA, Onesmo Kayanda amesema Vanessa Mdee ameshapatiwa kibali kaenda Afrika Kusini huku Gabo akipata kibali cha kwenda nchini Ireland.

Wii iliyopita Diamond Platnumz alizuiliwa kusafiri akiwa uwanja wa ndege baada ya kukiuka sheria hiyo na kutaka kusafiri bila kibali.