Harmorapa- Nimeumizwa Sana na Kitendo Cha Wema Kutangaza Ndoa

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Harmorapa amefunguka na kuweka wazi kuwa hisia zake zimeumizwa baada ya mwanamke anayempenda kutangaza Kuolewa na mwanaume mwingine.

Harmorapa ambaye amekuwa muwazi tangia Mwanzoni kuwa anampenda Wema na kutamani kuwa naye kimapenzi ameonekana kukata tamaa ya kuwa naye baada ya Wema kutangaza ndoa na mpenzi wake PCK.

Harmorapa ameeleza kuwa labda haikupangwa kwa yeye kuwa na Wema Sepetu ndio maana hadi sasa hajafanikiwa kuwa naye, hivyo amenyoosha mikono juu kuhusu hilo.

Siku chache zilizopita Wema alimuanika hadharani mpenzi wake PCK na kumuita Mume wake mtarajiwa lakini pia PCK amekiri kuwa anategemea kumuoa Wema hivi na inasemekana kuwa hivi sasa Wema yupo nchini Burundi kwa ajili ya kutambulishwa kwa ndugu wa PCK.

Kama Utakumbuka kuwa kwenye uzinduzi wa movie mpya ya Wema Sepetu, D.A.D uliofanyika Mlimani City wiki kadhaa zilizopita Harmorapa aliibuka na kumkabisha Wema zawadi ya ua kama ishara ya upendo wake kwake.

PCK Aweka Wazi Mipango Ya Ndoa na Wema

Mpenzi wa staa wa Bongo movie Wema Sepetu anayejulikana kama Patrick Christopher maarufu kama PCK ameibuka na kutangaza ndoa na Wema Sepetu.

Global Publishers wanaripoti kuwa Mahaba ni mazito kati ya Wema na PCK na kuwa Mrembo huyo atakuwa nchini Burundi kwa muda wa mwezi Mzima sasa kwa ajili ya kutambulishwa kwa ndugu wa PCK wanaoishi huko.

Lakini pia inaripotiwa kuwa Wema amekolea vibaya mno kwa mwanume huyo kiasi ya kwamba humaambii kitu lakini inadaiwa Familia ya Wema haimtaki PCK kutokana na taarifa za utapeli zinazosambaa Kwenye mitandao ya kijamii.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Risasi Mchanganyiko, PCK ameweka wazi kuwa ameshajitambulisha nyumbani kwa Wema na ndoa yao inatarajiwa kufungwa hivi karibuni mara tu watakapotejea Kwenye Safari yao ya Brazil walipo hivi sasa.

PCK amekiri kuwa atamuoa Wema Mke wa Pili kwani dini yake ya Kiislamu inaruhusu na kukiri  tayari ana Mke mmoja.

Lakini pia PCK amekana taarifa za yeye kuchukiwa na Familia ya Wema na kudai sio za kweli na kakataa tetesi za utapeli na hata taarifa za kufikishwa polisi baada ya yeye na Wema kutapeli watu.