Young Killer Athibitisha Kuachana na Miss Hip-Hop

Mwaka 2016 msanii wa musiki bongo  Young Killer wa Msodoki alitangaza kumuoa mwanamke aliyesema kuwa yuko nae katika mahusiano aliyekuwa akijulikana kama miss hip-hop, hali iliyofikia mpaka kumpachika jina ilo la miss hip-hop ikiwa kama ishara ya kuonyesha ni jinsi gani wamekuwa wakipendana.

Hata hivyo msanii huyo amefunguka hivi karibuni na kusema kuwa kwa sasa hayuko katika mahusiano ya kimapezni  na mwanadada huyo  tena kwaio maswala ya ndoa tayari yalishavunjika na hayupo katika mahusiano na miss hip hop  kwa takribani miezi sita sasa ilikwisha pita.

kulikuwa na kutokuelewana kidogo kati yangu na yeye swala lilipopelekea tusiwe pamoja kwa takribani miezi sita sasa. -Aliongea Young Killer

Akiongezea kwa kufafanua zaidi msanii huyo amesema kuwa sio swala la usaliti  hata kidogo lilowafanya waachane ila ni sababu za ndani ambazo hawezi kuziongelea zilizowafanya waachane.

Young Killer tangu alipotangaza yuko katika mahusiano na miss hip-hop , hajawahi kupata skendo yoyote ya kimapenzi na ndio maana hata walipoachana ilikuwa ni vigumu kujua kwa sababu ni moja ya wasanii waliaoamua kuweka mahusiano yao ya kimapenzi kuwa ni siri  zao katika maisha.

Young Killer Ametaja Kitu Kilichomuumiza Zaidi Kuhusiana na Harusi Ya Dogo Janja

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kurap Young Killer Msidoki amejiri kuwa amesikitishwa sana kwa kitendo cha yeye kutokuchangia kwenye harusi ya rafiki yake Dogo Janja.

Harusi ya Dogo Janja na Irene Uwoya iliwashtua watu wengi wiki chache zilizopita huku watu wengi wakibaki midomo wazi kutokana na tofauti kubwa iliyopo baina yao ya kiumri.

Kwenye mahojiano Young Killer aliyoyafanya na kituo cha televisheni cha East Africa amekiri kuwa ameumia kuwa hajachangia kwenye harusi ya janjaro:

Kilichoniuma zaidi ni kwa nini sijachangia harusi ya mwanangu hicho ndio kilicho-nipain lakini all in all nimefurahi kwamba janjaro ameoa kwa kweli ni kitu kikubwa sana kwa upande wake ni lazima apate furaha yake, kile kitu kinachomfanya awe na furaha lazima akifanye ili maisha mengine yaweze kuendelea lakini mimi pia ni mtu ambaye nilikuwa sijui nini kilikuwa kinaendelea nilijua kama watu wengine walivyojua nilikuwa surprised kuhusiana na harusi lakini nilikuwa nafahamu kuwa walikuwa na mahusiano”.

Kumekuwa na taarifa mbalimbali ya kwamba Dogo Janja, Young Killer na Young Dee wana bifu na hawapatani lakini Young Killer amekataa kuwa na bifu Dogo Janja:

Dogo Janja mimi ni mwanangu na tumekuwa tukizungumza vitu vingi kwaiyo nilikuwa nafahamu kuhusu uhusiano wake na Uwoya lakini sikujua kuhusu ndoa lakini nakumbuka baada ya ndoa alinitafuta mwenyewe na kunipa taarifa”.

 

Young D Kanizidi Tattoo Na Umri Lakini Kuchana Haniwezi- Young Killer

Msanii wa bongo fleva anayefanya miondoko ya kurap, Young Killer Msodoki amefunguka na kudai kuwa msanii mwenzake Young D hajamzidi kitu zaidi ya tattoo za mwilini lakini kwenye kurap na kuchana hawezi kumfikia hata siku moja.

Siku za hivi karibuni wasanii hawa wawili wamekuwa kwenye bifu zito sana la kurushiana maneno kwenye mitandao ya kijamii huku kila mmoja wao akidai ana uwezo mkubwa wa kuimba na kuchana kuliko mwenzake.

Katika mahojiano aliyoyafanya na Dizzim Tv, Young Killer alifunguka yafuatayo kuhusiana na bifu lake na Young D ambalo lilipelekea Young D kumtukana matusi ya nguo keen he kipindi cha Friday Night Live:

Unajua huu utamaduni wetu wa hip hop unaruhusiwa kumuweka mtu sawa kama hayupo sawa ili mradi haumtukani na vitu kama hivyo lakini mimi Young D alikuwa amenitukana matusi ya ndani kabisa, basi pale pale studio nikamuuliza akisema hataki kufananishwa na mimi anakuwa anamaanisha kwenye sekta gani labda? Lakini sikupata jibu ikabidi niseme tu ilimradi tupo studio DJ atuwekee biti tuchane, tumewekewa biti mi nimechana mwenzangu anaambiwa achane kuvhana hawezi basi hapo ndo wenyewe muone kuwa hatufai kufananishwa yaani unajiita rapa lakini kuchana huwezi basi mimi naona yeye alichonizidi ni tattoo mwilini na umri wake umeenda kidogo kuliko mimi lakini kuchana hawezi kunifikia hata siku moja nimeshamdhihirishia hilo”.

Young Killer ameongelea pia wimbo wake mpya alioshirikishwa na Diamond lakini pia aliongelea mchango mkubwa wa Fid q katika mziki wake na mafanikio yake kisanaa.

Alichosema Young Killer baada ya Diamond kuamua kutoa wimbo naye

Nyota ya Young Killer sasa inakaribia kung’aa vizuri, rapa huyo ataingia studio na Diamond Platnumz kurecord ngoma mpya itakayompa umaarufu nje ya Tanzania.

Msanii yeyote ambaye amewahi kufanya kazi na Diamond anajua vizuri thamani ya kumshirisha Simba kwa kolabo yoyote ile.

Young Killer

Young Killer sasa amefunguka kuhusu kazi atakayofanya na hit maker huyo wa ‘Marry You’. Rapa huyo alisema mama yake alifurahishwa sana na kitecho cha Diamond kuamua kumshirikisha kwenye moja kati ya nyimbo zake zinazokuja.

Akiongea na Bongo5 hapo jana Mai tarehe nne, Young Killer alimmwagia sifa Diamond na kumtaja kama msanii anayekuza vipaji Tanzania.

“Hiki kitendo kimenifanya nimuone Diamond Platnumz ni binadamu na ni mtu ambaye anastahili kuwepo sehemu ambayo yupo. Ni tukio ambalo limenitia faraja kiukweli hata mama yangu alivyosikia alifurahia sana na kumshukuru kwa kitendo ambacho amenifanyia,” alisema Young Killer.