Tanasha Afunguka Kila Kitu Kuhusu Maisha Yake

Mpenzi wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Tanasha Donna Oketh ambaye ana asili ya Kenya amefunguka mambo matano ambayo watu wengi hawajui kuhusu maisha yake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Jarida la Tag la nchini Kenya, Tanasha amefunguka mambo haya matano:

download latest music    

1. MISS WORLD KENYA

“Naitwa Tanasha Donna Barbieri Oketch a.k.a Zahara Zaire. Nina umri wa miaka 23. Mimi ni chotara. Mchanganyiko wa Mkenya na Muitaliano. Nimekulia Kenya. Niliondoka Kenya nikiwa na umri wa miaka 11 na kwenda Ulaya. Nikiwa Ulaya, nilianza kujihusisha na mitindo tangu nikiwa na umri mdogo. Nilishiriki maonesho mbalimbali likiwemo Miss Afrika-Ubeligiji. Baadaye nilirejea nyumbani Kenya, nilitaka kushiriki Shindano la Miss World- Kenya. Niliposhindwa ndiyo nikaweka makazi hapa nyumbani Kenya.

2. ELIMU

“Kuhusu elimu, baada ya shule za awali nilisoma masuala ya utalii nchini Ubeligiji. Nilijifunza lugha mbalimbali za kigeni. Ninaweza kuzungumza na kuandika lugha tano za Kingereza, Kiswahili, Kifaransa, Kidachi na Kihispaniola.

3. FANI

“Kwa sasa mimi ni mtangazaji wa redio (NGR ya Mombasa, Kenya). Ni video vixen (video queen ambaye aliuza sura kwenye Video ya Nagharamia ya Alikiba na Christian Bella).

4. HARAKATI ZA KUTOKA KIMAISHA

“Mimi ni mjasiriamali, nimewekeza kwenye bidhaa za urembo, ndiye mkurugenzi na mmiliki wa Kampuni ya For Her Luxury Hair inayosambaza bidhaa ya nywele.

5. UHUSIANO

“Ni kweli niliingia kwenye uhusiano wa Nick Mutuma (Mwigizaji wa kiume wa Kenya). Ulidumu kwa miezi saba tu kabla ya kuvunjika Agosti, 2017. Of course kwa sasa ni mpenzi wa Diamond Platnumz,” alikariri Tanasha na Jarida la Tag la nchini Kenya.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.