Tausi Aelezea Masikitiko Yake Baada ya Kumpoteza Mzee Majuto
Msanii wa maigizo, filamu na vichekesho nchini Tausi Mdegela alikuwa akionekana moja ya watu waliokuwa wakionekana kulia na kuumia sana siku ya msiba wa Mzee Majuto.Hata hivyo baada ya kuchunguza na kumhoji mwenyewe pia alikiri kuwa mzee majuto alikuwa baba yake wa hiari ambae pia ndie aliemfundisha sanaa na kumfanya awe hapa alipo.
Tausi anasema kuwa Mzee Majuto alikuwa kama baba yake mzazi kwa sababu ndie aliemlea na amekuwa akikaa kwake kwa muda mrefu sana kama mtoto wake wa kumlea mpaka kumfundisha sana na kuanza kujitegemea na ndoto kubwa ya mzee ilikuwa ni kumuona akifanikiwa na kufika mbali katika sana.
mimi hapa naumia sana kwa uchungu kwa sababu ya kumpotea baba yangu ambae kwa muda wote amekuwa akinifundisha sanaa na amekuwa akiaka kuniona kuwa nina fika mbali, na pia kila siku alikuwa akitaka kujua hali yangu kama mwanae.
Tausi pia ansema kuwa kabla mzee majuto hajafariki kua mtu alimpigia simu kumwambia kuwa mzee alikuwa anamwita na alikwenda kumuona na kumsikilia kabla hajakata roho.