The Mafik Wakumbwa na Kashfa ya Wizi.

Msanii wa kundi la The Mafik anayejulikana kwa jina la Mbalamwezi, amekamatwa na jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni kwa tuhuma za wizi.
Tukio hilo limetokea hapo jana baada ya msanii huyo kumuibia dereva wa gari moja ya kampuni zinazotoa huduma za usafiri binafsi jijini Dar es salaam (Taxify), aliyejulikana kwa jina la Calvin.

Akisimulia tukio hilo Calvin amesema Mbalamwezi aliitisha usafiri akitumia simu ya mwenzake, lakini alipokuwa njiani alionekana kuwapigia simu watu kuomba hela kwani hakuwa na pesa ya kumlipa dereva, na ndipo alipochukua uamuzi wa kumuibia dereva baada ya kumfanya apoteze fahamu.

download latest music    

Wasanii hawa wa kundi la The mafik kwa sasa wamekuwa na mashabiki wenhgi na kama swala hili ni kweli basi inaweza hata kuharibu upendo kwa mashabiki wao.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.