TID Ajikanyaga Kutoa Majibu Kuhusu Ushirikina

Msanii mkongwe wa muziki wa Bongo fleva Khalid Mohamed maarufu kama Top In Dar, TID amejikuta akipata kigugumizi pale alipotandikwa maswali kuhusu mambo ya kishirikina.

Siku za hivi karibuni topic ambayo imekuwa ikitrend Kwenye mitandao ya kijamii ni suala zinasambaa la uchawi ambapo watu maarufu wamekuwa wakinyosheana vidole kuhusu ushirikina.

download latest music    

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha habari, TID alipoulizwa kuhusu uchawi alishindwa kutoa jibu la moja kwa moja na kuishia kupata kigugumizi na kudai haamini uwepo wa masuala ya ushirikina katika muziki hususani kwa wasanii, kwa sababu hajawahi kuona wala kuletewa ushahidi kuhusu mambo hayo.

Nikiulizwa swali kama hilo, mnanichanganya maana mimi sina utaalam wa hayo mambo. Nitafutieni ushahidi niufanyie upembuzi ili niweze kujua kama kweli washirikina wapo au laa”.

Lakini pia Msanii mwingine wa Bongo fleva Dayna Nyange alipotandikwa swali hilo hilo aliweka wazi kuwa uchawi upo kwa sababu hata kwenye vitabu vya dini imeandikwa hivyo.

Uchawi upo kiukweli, itabidi nimtafute TID ili niongee naye kwanini hajui masuala ya ushirikina”.

Siku mbili hizi zilizopita Hamisa Mobetto ametrend sana Kwenye mitandao ya kijamii kwa kutuhumiwa kuwa anafanya mambo ya kishirikina.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.