TID Amtupia Dongo Diamond Kwa Kujiita Simba

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva Khalid Mohamed maarufu kwa Jina la usanii kama Top In Dar (TID) amedai yeye ndiye mwanzilishi wa jina la mnyama.

Hivi siku za karibuni kumekuwa na ugomvi wa marina baina ya wasanii kama juzi tu Afande Sele kamaliza mgogoro na Diamond kisa jina la Simba ambalo kila moja alidai la kwake.

download latest music    

TID ameibuka na kudai yeye ndiye mwanzilishia wa kutumia jina la Simba na hata kudai jina hilo alipewa na mashabiki zake kwa sababu ya kazi zake anazofanya akiwa stejini.

Kwenye mahojiano na kipichi cha On The Street cha ETV, TID amefunguka haya kuhusu jina hilo la mnyama:

Kwa mfano mimi perfomance zangu wanasema ni kali, yaani za kinyama, kwahiyo mimi nilikuwa nafanya kinyama ndipo mashabiki walipo amua kunipa jina la mnyama, mpaka sasa mimi ni mnyama kutoka unyamani.

Lakini sio mbaya sasa hivi nasikia kuna wengine wanajiita Simba, nimewa-inspire kuwa hivyo, kuna wengine ni wakufungwa, lakini ndio mnyama wenyewe”.

TID hana uhusiano Mzuri na WCB kwa ujumla kwani wiki chache tu zilizopita alitoka kutoa povu kwa Wasafi baada ya kudaiwa alikuwa anaomba kazi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.