TID- Kuna Watu Wanataka Kumshusha Diamond

Mkongwe kwenye muziki wa Bongo fleva Khalid Mohamed maarufu kama TID amefunguka na kuwatolea povu baadhi ya media ambazo zinadai a kumshusha staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

TID amedai kuwa kwa muda mrefu kumekuwa kuna utaratibu wa wadau wa muziki wa Bongo fleva kujaribu au hata kumshusha kabisa msanii pale anapothubutu kudai maslahi yake jambo ambalo amedai linaua muziki.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, TID amejilinganisha na Diamond na kudai hata yeye ilishawahi kumtokea Kwenye muziki wake ambapo kuna baadhi ya vyombo vya habari vilijaribu kumshusha.

Na kweli anaweza because he has a media, yaani yeye ndio kama Mungu anajiona but mimi hapana. Nilifanya kosa hilo lakini kosa hilo ndilo limewasanua wasanii wengine, unaona msanii kama Diamond naye amekataa.

So Diamond was me lakini wakasema wewe siunajifanya mjanja sasa tunamleta Diamond tukushushe wewe. At the end Diamond naye wanataka kumuua, sijui wanataka kumuweka nani,” TID ameiambia Wasafi TV“.

Diamond ni moja kati ya wasanii ambao wamekuwa Kwenye migogoro na baadhi ya vyombo vya habari kama Clouds Fm na East Africa Tv ambavyo havipigi kabisa nyimbo zake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.