Tigo Fiesta 2018 Kuanzia Morogoro.
Tamasha kubwa nchi ambalo huwakutanisha wasanii na mashabiki wao kwa ukaribu zaidi wakiwa wengi zaidi la Tigo Fiesta linatarajiwa kuanza hivi karibuni baada ya kuzinduliwa siku ya jana huku mwaka huu wakiamua kuanza na mkoa wa Morogoro.
Tamasha hilo ambalo pia huwa na manufaa na maendeleo katika jamii kutona na kuleta huduma za muhimu karibia kila sehemu wanazopita linangojewa namashabiki kwa hamu kutokana na ukubwa wake lakini pia kwa sababu limekuwa likiwakutanisha wasanii wengi kwa wakati mmoja.
Hata hivyo tamasha hili linatajwa kuwa ndio tamahsa kubwa kuliko matamasha yote Afrika Mashariki .