Tunda aeleza kwanini hatoweka mambo ya mapenzi yake kwenye mitandaoni kama zamani

Image: Tunda

Mrembo Tunda ambaye anajulikana kutokea kwenye video za wasanii wakubwa wa bongo amefunga kusema kuwa kwa hivi sasa hatamani mapenzi ya mitandaoni. Hapo mbeleni alikuwa akitoka kimapenzi na Young D lakini baada ya mambo kadhaa wawili hawa waliachana na kila mmoja kwenda njia yake.

Tunda
Tunda

Akizungumza na Uwazi Showbiz hivi karibuni mrembo huyu alisema kuwa uhusiano wake na Young D ulikuwa sana mitandaoni kitu ambacho hakuwa anajua inaweza kuleta utata.

download latest music    

Hata hivyo kulingana na yeye, hatorudi kufanya hivi tena kwa sababu amejua kuwa sio marafiki wake wote wanamtakia mazuri na badala ya kumueka mpenzi wake mitandaoni anaonelea kukaa kimya. Alisema,

“Kiukweli nimejifunza juu ya kuwa muwazi katika suala zima la mapenzi kuwa kuna watu wengine hawapendi kuona mnakuwa na furaha.Hawa huweza kupenyeza maneno ya kuwagombanisha ilimradi tu muweze kuachana, sasa mimi nimeamua katika uhusiano wangu wa sasa kutokuwa muwazi, mtu anayefahamu juu ya ninatoka na nani kwa sasa lazima atakuwa amefanya kazi ya ziada.”

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua