Tunda aeleza sababu ambazo wasanii wengi hawatoi nyimbo baada ya kufunga ndoa

Tunda ambaye ni msanii mkubwa kutoka Bongo amefunguka kuelezea sababu ambazo wasanii wengi hukawia bila kuachia muziki baada ya kuoa.

Msanii huyo aliambia Bongo 5 kuwa wasanii wengi hukawia ndio warejelee na nyimbo ambazo wake zao na jamii wanaweza kusikiza. Aliendelea kwa kusema kuwa kuna wasanii Kama Mr Blue ambao wameweza kuachia nyimbo zinazofanya vizuri hata baada ya kupata bibi.

download latest music    

Alisema,

“Msanii akioa eti anapotea kwenye muziki hizo ni dhana potofu, kuna wasanii wengi wameoa na bado wanafanya vizuri, wapo akina Mr Blue wanafanya vizuri. Mimi najua msanii anaweza kupotea kama anatoa nyimbo za kumuimbia mke wake, mke wako unatakiwa kumuimbia ndani mwako, na jamii inataka muziki wao,”

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua