Tunda Akumbwa Na Skendo Ya Mimba Kwa Mara Ya Pili

Sio mara ya kwanza kwa muuza nyango maarufu katika video mbalimbali kuambiwa kuwa anamimba,Tunda ambae miezi kadha iliyopita alisemekana kuwa na mimba lakini baadae ilisemekana kuwa ametoa mimba hiyo bila kuweka wazi ni nani alikuwa muhusika wa mimba hiyo.

Hata hivyo mwanadada huyo alisema kuwa hakuna na mimba ya mtu yoyote na kitendo chake cha kuwa na mwili mkubwa ni kunenepa kwa sababu amekuwa akila sana vyakula lakini alisema anaanza kufanya diet ili kupunguza mwili huo, na kusema kuwa alikuwa hajui swala lolote kuhusu mimba watu wamekuwa wakimsingizia.

download latest music    

Hivi karibuni tena , mwanadada huyo ameonekana akiendelea kupasuka kutokana na badahi ya sehemu za mwili wake kuendelea kuongezea kama tumbo pamoja na maziwa ambapo waatalamu wa mambo wanasema kuwa mwanadada huyo kwa sasa ana mimba na hawezi kupindua hilo.lakini kitu cha kushangaza ni kwamba mwanadada huyo amekataa na kusema kuwa hana mimba.

Lakini pia mwanadada huyo amekataa kuzushiwa kuwa mimba aliyonayo ni ya msanii wa bongo fleva  ambae alikuwa mpenzi wake wa muda mrefu kwa kipindi cha nyuma, na kusema kuwa kitendo cha yeye kumuweka katika ukurasa wake wa instagram mara nyingi ni kwa sababu anamsapoti msanii huyo kama rafiki yake na sio vinginevyo kama watu wamekuwa wakimzushia.

Ndio kwanza nasikia kwenu mimi wala sina mimba, na wala hizo taarifa sio za kweli kabisa.Huwa namuweka insta ili kusapoti kazi zake tu maana ni rafiki yangu sana sana lakini cha ajabu watu walivyoona hivyo tu ndo wakaanza kuzusha  kwamba ninatoka nae na nina mimba yake , swala la kuhusu kunenepa ni kweli nimenenepa sana kwa sababu nimeridhika na maisha ninayoishi tu.

Hata hivyo Tunda amekuwa kila siku akikana swala la yeye kuwa na ujauzito huku wataalamu wa mambo wakisem akuwa mtu mjamzito akionekana anaweza kujulikana kutokana na vile anavyokuwa.Kama ni kweli mjamzito tunamtakia afya bora yeye na kiumbe kilichopo tumbano na kama ni uzushi basi kila la kheri kwake.Maana wahenga wanasema lisemwalo lipo kama halipo linakuja.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.