Tunda Anapenda Sana Kufatilia Maisha Yangu Binafsi: Petit Man

Petit Man Wakuache ambaye ni mume wa dada wa Diamond, Esma Platnumz amefunguka kuhusu skendo iliyomwandama wiki chache zilizopita pale alipomtolea matusi ya nguoni mrembo Tunda.

Petit Man alipata umaarufu kwa mara ya kwanza alipokuwa na ukaribu na mrembo Wema Sepetu. Baada ya kumuoa Esma na kuwa shemeji wa Diamond ndipo pale umaarufu ulipozidi. Lakini muda wote Petit aliweka ukaribu wake zaidi na Wema kuliko na familia ya Esma, lakini hata baada ya kupatana na Wema siku za hivi karibuni Petit ameonekana kuweka ukaribu zaidi na familia ya Diamond.

download latest music    

Tunda ambaye amekuwa na urafiki wa siku nyingi na Petit Man alirushiwa matusi hayo na Petit baada ya kumuita Petit chawa wa Diamond baada ya Petit kusafiri na timu nzima ya Diamond kuelekea Zanzibar kwaajili ya shoo ya Diamond. Kitendo kile cha kuitwa chawa na Tunda kilimuumiza Petit na kumtukana Tunda.

Alipohojiwa na clouds tv Petit alifunguka yafuatayo kuhusiana na Tunda:

Yaani yule msichana Tunda anapenda sana kuingilia vitu vyangu binafsi yaani anachimba vitu vyangu vya ndani sana anapenda kuviingilia na kuviongelea sasa sielewi kwa nini anapenda kunizungumzia wakati mimi simzungumzii hata siku moja kwaiyo kitu kama hicho kinatokea kea binadamu yoyote unaposikia unazungumziwa kitu kibaya kupaniki kitu cha kawaida sana”.

Pia Petit alifunguka kuwa kwa sasa anasimamia wasanii wawili ambao ni Country Boy na Bill Nass ambao wanategemea kutoa kazi zao mpya hivi karibuni.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.