Tunda Aomba Msamaha Kwa Petitman

Tunda na Petiti Man walikuwa katika bifu zito baada ya Tunda kumwita Petit kuwa chawa wa Wcb, lakini bifu hilo halikuishia hapo liliendelea na kufikia hatua ya watu hao kutukanana katika mitandao ya kijamii na  baade kuna baadhi ya  ya sms zilivuja zikionyesha wawili hao kuwa wamekuwa wakitukanana hata katika magroup ya whatsap na katika simu zao.Hata hivyo mwanadada huyo aliamua kukubali yaishe na kuamua kujishusha kwa kuomba msamaha kwa Petitman

Hata hivyo akiongea na Clouds E ya Clouds Tv, mwanadada Tunda amesema kuwa yeye ameamua kuomba msamaha na bora aishe kwa sababu yeye ni muoga sana wa kuwa na bifu na watu na anaogopa sana kupigwa hivyo aliona bora yaishe kuliko kuanza kuangalia ni nani kamkosea nani.

download latest music    

Niliamua kuona bora yaishe kwa sababu sitaki kuwa na bifu na watu, mimi sitaki kujua  nani kamuanza mwenzake lakini bora tu bifu liishe kwa sababu mimi ni muoga sana wa mabifu alafu naogoapa sana kupigwa kwaiyo sitaki tu. -Alisema Tunda

Hata hivyo aliulizwa kwanini waligombana mpaka kufikia hatua ya kuyaanika katika mtandao Tunda anasema kuwa bifu hilo halikuanzia instagram lakini lilianzia private katika simu zao na baadae watu walikuja kuvujisha katika mitandao ya kijamii, bila hata  kujua nini chanzo.

Akiendelea kuongezea , mwanadada huyo anasema kuwa watu wengi wamekuwa wakimjudge kutokana na maisha yake anayoishi  na kuyaweka katika ukurasa wake wa instagram lakini ukweli ni kwamba hayo sio maisha yake kuna muda huweza kujisikia akaposti   kitu chochote lakini sio kwamba ndivyo anavyoishi kila wakati.

Alipoendelea kuulizwa kuhusu tabia yake ya kuonekana katika viwanja na kula bata mwandada huyo anasema kuwa watu wamekuwa wakimsema kuwa anafanya starehe sana na hata wengine kumuiga maisha anayoishi yeye bila kujua yeye ela anatoa wapi, ni bora kila mtu akaamua kuishi maisha yake na sio kuanza kuiga maisha anayoishi yeye kwa sabau kwake yeye starehe ni kitu cha kawaida kutokana na ela anayoingiza ingawa kuna muda huwa anakaa nyumbani tu na kupika na kula lakini akiamua kutoka na kuspend kwa chakula huwezi kufika hata milioni moja na nusu.

Huwa nakaa nyumbani najifungia na kupika na kula lakini nikiamua huwa naweza kutumia hata milioni moja na nusu kwa ajili yaku-spendi kwa siku.-Alifunguka Tunda

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.