Tunda- Nipo Tayari Kuwa Mke Wa Mtu

Muuza nyago maarufu mtandaoni Tunda Sebastian maarufu kama ‘Tunda the Bossbabe’ amefunguka na kudai kuwa hivi sasa ametulia na yupo tayari kuwa mke wa mtu.

Siku za hivi karibuni Tunda ameonekana kubadilika sana kwani kwa mara ya kwanza alipata umaarufu kwenye mitandao ya kijamii kwa vituko vyake vya kuvaa nguo za utupu na kula bata ndefu ambapo watu walikuwa wanamweka kwenye kundi moja na warembo kama Gigy Money.

download latest music    

Pamoja na hayo ni mara kwa mara kumekuwa na tetesi kuwa Tunda ni mjamzito ingawa mwenyewe amekuwa akikataa mwaka jana mwishoni habari zilienea kuwa Tunda ana ujauzito wa msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz ingawa mwenyewe alikataa tuhuma hizo na kudai kuwa watu wengi walidhani kuwa ni mjamzito kwa sababu alinenepa na kuwa na kitambi lakini sababu pekee iliyopelekea yeye kunenepa ni kula sana na si kingine.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Star Mix hivi karibuni Tunda amefunguka kuwa anapendezwa na muonekano alionao hivi sasa kwani angalau anaonekana mtu mzima kiasi ya lwamba mtu akimuona anaweza jua ni make wa kuia na kuweka ndani.

Nafurahia sana muonekano wangu wa sasa hivi nilivyo na kwa sasa nipo tayari kuitwa mke wa Mtu maana hata nikiwekwa ndani kama mke nafaa kabisa nilikuwa nakereka watu kunifananisha na katoto kadogo”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.