Tunda- Sina Bifu na Hamisa

Video vixen maarufu Kwenye mitandao ya kijamii Tunda Sebastian ameibuka na kuweka wazi kuwa hana bifu lolote na Hamisa Mobetto na wala hajawahi kugombana naye.

Tunda na Hamisa walisemekana lies Kwenye bifu zito siku za nyuma na ikidaiwa kisa kilikuwa ni penzi la staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz.

download latest music    

Inajulikana wazi kuwa Hamisa ana uhusiano na Diamond na hata kuzaa naye mtoto mmoja lakini hapo nyuma ilishasemekana kuwa Tunda alikuwa ana uhusiano na Diamond kwa muda mrefu.

Kuwepo kwa bifu hilo kulithibitika baada ya Tunda kutumia mtandao wa kijamii kumfikishia Ujumbe Hamisa Miezi kadhaa iliyopita na kusema kuwa Diamond hamtaki lakini anajipendekeza.

Lakini pia siku zilizopita Tunda alimpiga Dongo Zito Hamisa baada ya kusikia karudisha majeshi kwa Diamond ambapo alidai ni mjinga kwa kurudiana na Diamond.

Siku ya juzi Tunda kawatolea povu zito watu walioandika stori kuwa yeye na Hamisa wana bifu ambapo amedai kuwa hana ugomvi wowote na Hamisa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Tunda aliandika ujumbe huu huku akisisitiza kuwa hana bifu na Hamisa:

Hamisa hajawahi kujibu tuhuma zozote na Tunda na hata kumrushia maneno Kwenye mitandao ya kijamii.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.