Tundaman- Bob Junior Ni Mtoto Mdogo Sana Kwangu

Mwanamuziki mkongwe wa Bongo fleva Tundaman ameibuka na kumtolea povu zito msanii mwenzake Lakini pia producer wa muziki Bob Junior na kudai ni mtoto mdogo sana.

Tunda man ni moja kati ya wasanii ambaye ameshawahi kufanya vizuri sana siku za nyuma na kazi zake lakini kwa muda mrefu amekuwa kimya na hajasikika akitoa ngoma na Ametaja Sababu kuwa ni ndoa yake na mtoto wake.

download latest music    

Baada ya kimya kingi Tunda amerudi kwa kasi ya ajabu kwani wiki iliyopita aliachia ngoma zake tatu mfululizo pamoja na video zake kwenye kipindi cha Friday Night Live.

Lakini baada ya tukio hilo Bob Junior ameibuka na kudai kitendo cha Tundaman kutoa video tatu kwa mkupuo mmoja ni kukurupuka bila kuangalia hali ikoje.

Kwenye mahojiano na Enews ya East Africa Tv, Tunda man amemjia juu Bob junior na kumuita bwana mdogo sana kwake kwaiyo hawezi kumwambia kitu:

Mimi na Bob Junior ni vitu viwili tofauti Kwanza mimi nimeanza kufanya Muziki muda mrefu Bob Junior kaja juzi juzi tu hapa 2009 sijui 2010 kwaiyo Kwenye muziki hawezi kunishauri kitu chochote kikaendana na mziki wangu ni bwana mdogo sana kwangu”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.