Uchebe Akana Kumpiga Shiloleh.
Mume wa msanii Zuwema Mohamed maarufu kama Shiloleh anaejulikana kama Uchebe amefunguka na kuongelea swala la yeye kumpiga mwanamke wake baada ya kusambaa kwa maneno katika mitandao ya kijamii kuwa inawezekana wawili hao wamegombana baada ya kutokea kwa ugomvi mkubwa ambao ulisababaishwa na Sudy Brown.
Uchebe anasema kuwa watu wengi wamekuwa wakimuona kaka yeye mi mtu baunsa na kwamba anaonekanakuwa anampiga mke wake kila siku lakini ukweli ni kwamba hajawahi kumpiga mke wake huyo hata siku moja tangu amemuoa na maneno yanayosema hayana ukweli wowote.
Watu wengi wananiona kama mimi ni mtu wa kupiga piga tu,lakini ukweli ni kwamba siwezi kumtandika mke wangu hata siku moja.-Alifunguka Uchebe
Waandishi wa habari waliamua kumtafuta Shiloleh ili kumuuliza kama zile habari za kuwa wanaugomvi na mume wake na kwamba alipigwa hadharani kama zina ukweli wowote , lakini shiloleh alikataa na kusema kuwa hakuna kitu kama icho.