Ujio Mpya wa Alikiba kwa Mashabiki Zake, Haja na Hela.
Msanii ambae alisumbua na kutia wasiwasi watu wengi amerudi kwa kishindo huko akiwaweka mshabiki zake katika mkao wa kusubiria baada ya kuweka katika ukurasa wake wa instagram picha ya wimbo wake mpya ambayo inakuja kwa jina la Hela.
Alikiba ambae hapo awali watu walisema kuwa uenda msanii huyo ameamua kufanya mpira na sio muziki tena kutokana na kuonekana akiwa amesajiriwa katika timu ya coastal uniona na kaunza kucheza mechi za ligi zinazoendelea hivi sasa.
Akiandika katika ukurasa wake wa instagram Alikiba aliweka picha yenye kuonyesha kuwa kuna kitu kipya kinakuja .
Hata hivyo imezoeleka kuwa msanii huyo anapotoa wimbo mmoja utumia muda mwingi sana mpaka kuja kutoa wimbo mwingine , huku kwa kipindi hiki hali imekuwa tofauti kidogo kutokana na kwamba kwa sasa muda wa kuwasubirisha mashabiki umekuwa mdogo.