Ujumbe wa Roma Mkatoliki kwa wasanii wa Bongo: Muache kutegemea media

Roma Mkatoliki ametoa ujumbe kwa wasanii wa wenzake, staa huyo anayetamba kwa wa wimbo mpya ‘Zimbabwe’ amewataka wasanii wa Bongo waache kutegemea media kupush ngoma zao.

Akiongea na The Playlist ya Times FM, Roma alisema kuwa kuna baadhi ya wasanii ambao wanapata upendeleo wa ngoma zao kupata airtime katika media.

download latest music    

Rapa huyo alionya kuwa mtindo huo ni hatari kwani wasanii hao wanapobwagwa na media mara nyingi huwa wanavyoshindwa kuishi kabisa.

“Yeah, off course asilimia mia moja kuna wasanii wanabebwa na media na pale media inapokata mirija utaona the way wanavyoshindwa kuishi kitu ambacho si kizuri, nashauri mtu atumie kipaji chake halafu aweze kujua at any time unaweza ukabwagwa na media halafu ukatakiwa usimame wewe kama wewe sasa kitaa unacho?, kwa sababu mimi naamini cha kwanza kitaa. Kitaa kikikuelewe media ni bless tu, utakuta ni Miaka minne/mitano wimbo wangu haujaingia kwenye chart za top ten lakini nikidondoka kwenye show na huo wimbo, bwana wee!!, kwa hiyo ile show yangu ya Mbagala ndio top ten yangu,” Alisema Roma.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere