Ukaribu na Wema Sepetu Wamponza Diana Kimary

Msanii wa fialmu za Bongo movie mrembo Diana Kimary amefunguka na kuweka wazi kuwa hajali manneo ya watu ambayo yamekuwa yakusemwa kuhusu yeye kuwa na ukaribu na Wema Sepetu ambapo amedai hajali na acha waendelee kumnanga lakini hawajui maisha yake halisi.

Diana Kimary ameonekana kuwa karibu sana na Wema Sepetu ambapo amekuwa akimuita dada lakini ukaribu huo umekuwa ukiibua maneno mengi sana  kwenye mitandao ya kijamii na kupelekea kusemwa sana na mashabiki.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na gazeti la Ijumaa, Diana alisema kuwa watu wengi kwenye mitandao ya kijamii hawajui kabisa maisha halisi ya mtu zaidi ya kukisia na kumsema vyovyote wawezavyo ndio maana hawafuatilii.

Unajua ni hivi wamenisema sana hapa katikati lakini hawajui kamwe maisha yangu na uzuri najitambua havinisumbui kabisa najua nini nataka maishani mwangu kwa hiyo hata kama wakinitukana ni sawa kwa vile siwalipii bando”.

Diana amekuwa na ukaribu na Wema kwa kipindi sasa ambapo ukaribu huo umemfanya hadi kujichora tattoo yenye jina la Wema.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.