“Unajiona Mzuri na Mdogo Lakini Huwezi Kupata Mwanaume Wako” Zari Amrushia Hamisa Dongo

Mfanyabiashara na mzazi mwenza wa msanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan ‘Zari’ amerudi tena kwenye headlines baada ya kumua kufumua bifu lake na baby mama mwingine wa Diamond, Hamisa Mobetto.

Inaelekea bifu la wazazi wenza wa Diamond  limerudi upyaaa kwani Zari kaamua kulianzisha tena baada ya kimya kirefu juu ya suala hilo na tofauti tulivyodhani kuwa huenda wamemaliza tofauti zao kama ambavyo Diamond na Hamisa walivyomaliza mahakamani.

download latest music    

Siku ya jana Zari kutumia mtandao wa SnapChat alimrushia Hamisa madongo upya kama ilivyokuwa siku za nyuma ambapo ameongelea kuhusu suala la Hamisa kuzaa na Diamond na pia taarifa za Hamisa kuchumbiwa na Diamond.

Siku za nyumba Hamisa ameshawahi kudokeza kuwa aliwahi kuchumbiwa au kuvalishwa Pete ya uchumba na Diamond na hata kuna taarifa zilienea kuwa huenda Diamond na Hamisa walifunga ndoa habari ambazo hazijawahi kuthibitishwa.

Mzuri, Mdogo lakini pamoja na hayo yote huwezi kupata mwanaume wa peke yako…..Eti amekuvalisha pete ya uchumba lakini hajawahi kukubali wala kukukubali hadharani! Dada jiangalie sana ….Anafanya Interview redioni eti mwenye mimba atoke blah blah”.

 

Lakini ni pia Zari ametangaza ujio wa kipindi chake kitakachoonyesha maisha yake halisia (reality show)  kitakachoitwa Life of Zarithebosslady ambacho mashabiki wake watapata kuona kila kitu kuhusu maisha yake.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.