“Unaonekana Hushindwi Hata Kumuua Mama Yangu” Diamond Amshukia Hamisa Baada Ya Skendo Ya Uchawi

Staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz amemshirikisha mzazi mwenzake Hamisa Mobetto baada ya skendo za kumloga kwa waganga kupamba moto.

Sakata hilo limetokea baada ya voice note zilizomuhusisha Hamisa na mama yake wakiwa wanazungumza na mganga kusambaa Kwenye mita ya kijamii.

download latest music    

Kwenye voice note hizo Hamisa anasikika akimuomba mganga amfanyie dawa ambayo itamfanya Diamond ampende na amuoe na Mama Diamond na Familia yake imkubali kama zamani.

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, Diamond amefunguka kuhusu sakata hilo na kumwagia povu zito Hamisa:

Unapotaka kwenda kwa mganga uniroge mimi na mama yangu, unaonekana wewe haushindwi hata kumuua mama yangu, kama unawaza sijui nikupe nyumba. Voice notes zinasambaa sambaa hata mimi nilitumiwa, ninazo unasikia kitu halafu unajua huyu ni yeye, halafu nikamwambia huyu ni wewe.

Watu kuna vitu wanaongea ongea halafu wanajaribu kuvipindisha aonekane Mama yangu na dada yangu wana matatizo, mama yangu na dada yangu hawawezi kuwa na matatizo. Halafu hao watu wako unaowatuma wakatukane nimeshakuona ukiwatuma wakatukane kwa watu wengine kwa sababu pia uliwatuma pia wamtukane na Zamaradi”.

Wiki hii dada wa Diamond Platnumz, Esma aliandika ujumbe mrefu kukanusha taarifa ambazo zilikuwa zinasambaa kwenye mitandao kwamba wameandaa voice note kwaajili ya kumchafua Hamisa Mobetto.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.