Uongozi Wa Coastal Union Utamruhusu Ali Kiba Kuendelea na Ratiba za Kimuziki

Staa wa Muziki wa Bongo fleva Ali kiba amefanikiwa kusajiliwa rasmi katika kuichezea soka la kulipwa timu ya Coastal Union ya mkoani Tanga.

Uongozi wa klabu ya Coastal Union umethibitisha kukamilisha usajili wa Alikiba ambaye amesaini mkataba wa mwaka mmoja kwa ajili  kuitumikia timu hiyo msimu ujao wa ligi kuu soka Tanzania Bara.

download latest music    
.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Championi Ijumaa, meneja wa timu hiyo, Said Hilary alisema Ali Kiba ni mchezaji mzuri na ameenda kwenye timu ya mpira na lengo lao kubwa ni kuitangaza Coastal.

Tumemsajili kwa mkataba wa mwaka mmoja na tunafahamu yeye ni mwanamuziki kwa hiyo akiwa na shughuli zake za kimuziki ataendelea na shughuli zake kama kawaida na akiwa yupo huru basi atacheza kuisaidia timu maana tuna uamini uwezo wake ndiyo maana tumemsajili“.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.