Uwoya Afungukia Skendo Ya Dogo Janja na Wema Sepetu

Msanii wa filamu za Bongo movie mrembo Irene Uwoya amefungukia skendo ambayo ilikuwa inamkabili aliyekuwa mume wake staa wa Bongo fleva Dogo Jnja na Bongo movie star Wema Sepetu.

Wiki chache zilizopita habari zilienea kuwa ndoa ya Uwoya na Dogo Janja imefika mwisho baada ya Dogo Janja  kubanjuka na Wema Sepetu wakati bado akiwa kwenye mahusiano na Irene Uwoya.

download latest music    

 

Katika mahojiano na gazeti la Risasi Jumamosi, Uwoya amesema kuwa, hakuwa na muda wa kuwauliza chochote kwa sababu wote ni watu wazima. Uwoya amesema hana mpango wowote wa kuongea chochote kuhusiana na madai hayo kwa sababu kama waliamua kufanya hivyo (kutoka kimapenzi) ina maana hawakuwa vichaa, bali waliamua na walikubaliana hivyo kwa upande wake hawezi kufanya chochote.

Unajua mimi nipo bize, ninafanya mambo yangu, halafu tena nitenge muda mwingine wa kuwahoji watu wazima wanaojitambua kuwa kwa nini waliamua kutembea na kufanya mapenzi? Kwangu mimi hapana kabisa… sina muda huo, wangekuwa hawana akili nzuri ningesema sawa, lakini ni watu wenye akili timamu kabisa”.

Lakini pia Uwoya ameweka wazi kuwa yeye aliishia kuwatazama tu ili aone mwisho wao utakavyokuwa hivyo anashukuru mambo yamekuwa hadharani kwani yeye ndiye alikuwa akionekana mkorofi siku zote.

Alisema katika hali kama hiyo yeye aliishia kuwatazama tu ili aone mwisho wao utakavyokuwa hivyo anashukuru mambo yamekuwa hadharani kwani yeye ndiye alikuwa akionekana mkorofi siku zote.

Niliamua kuwaangalia tu mpaka mwisho kwani nina vitu vingi vya kufanya ambavyo vinaniumiza sana kichwa changu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.