Vanessa Atoa Siri Ya Uhusiano Wake na Jux Wakati Bado Yupo na Jack Cliff

Staa wa Muziki wa Bongo fleva Vanessa Mdee ‘Vee- Money’ ameweka wazi kuwa alikuwa anawasiliana na Jux wakati bado yupo Kwenye Mahusiano na Jack Cliff.

Jux ambaye amekuwa Kwenye Mahusiano na Vanessa kwa muda sasa lakini siku za nyuma alishawahi kufaidi penzi na Jack Cliff aliyekuwa Miss Tanzania ambaye kwa sasa anaozea gerezani nchini China baada ya kukamatwa na madawa ya kulevya.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, Vanessa amefunguka  kuwa wakati Jux akiwa kwenye mahusiano na Jack alikuwa anakaaa naye studio wakirekodi lakini kama rafiki tu ingawa Jack alikuwa anaona wivu.

The first time nakutana naye alikuwa na jacky halafu kipindi hiko nikiwa studio na Jux, Jacky alikuwa anapiga simu sana anauliza yuko na nani lakini hiyo ilikuwa kabla ya kuwa Kwenye Mahusiano, nakumbuka alikuwa ananipeleka studio enzi hizo mimi sina gari na Jux alikuwa na bonge la ndinga”.

Jux na Vanessa wapo katikati ya Tour yao ya ‘In Love and Money’ ambayo imeendelea kufanya vizuri katika mikoa mbali mbali.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.