Vanessa Mdee Afungukia Tetesi Za Kumwagana na Jux

Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini Vanessa Mdee ‘Vee Money’ Amefunguka na kuweka wazi hali ya mahusiano yake kwa sasa na Mpenzi Wake Juma Jux.

Siku za Hivi karibuni kumekuwa na tetesi kuwa kapo kali kutokea katika tasnia ya Bongo fleva yaani na Vanessa na Jux wameachana baada ya wawili hao kutoonekana pamoja kwenye mitandao ya kijamii kwa kipindi kirefu sasa.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Vanessa Mdee ameamua kufunguka baada ya tetesi kuzagaa amemwagana na Jux kwa sababu amemsaliti, Vee Money amesema hana tatizo kabisa na Jux ila kazi ndiyo zinazowafanya wasiwe karibu hivyo watu kuona kama hawapo sawa.

Mimi na Jux hatuwezi kuwa pamoja kila siku kuna kipindi kazi zinabana sana na ndio maana watu wanaona tumemwagana, niwatoe hofu tu mashabiki zangu kwamba tupo sawa na hakuna kitu chochote kibaya kinachoendelea kati yetu zaidi ya ubize wa kazi unaotufanya tuwe mbali”.

Vanessa na Jux wameshakuwa pamoja kwa zaidi ya miaka mitano hapo kati waliachana lakini walirudiana Baada ya kusameheana.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.