Vanessa Mdee Amejiunga na Universal Music na Kupata Dili La Mkwanja Mrefu Haijawahi Kutokea

Mwanamuziki wa Bongo fleva Vanessa Mdee amezidi kupata mafanikio yasiyo na kipimo baada ya kupata deal jipya la mkwanja mrefu na kampuni ya Universal na Air force 1.

Mwaka 2017 umezidi kuwa mzuri kwa supastaa huyo kwani huu sio mkataba wa kwanza Vanessa amesaini na kupata mkwanja mapema mwaka huu alipata nafasi ya kuwa balozi wa Hyatt Regency.

download latest music    

Siku ya Jana mchana Vanessa kupitia ukurasa wake wa Instagram alitangaza habari njema kuwa zitakuja punde na hivyo baadae aliweka wazi mafanikio hayo aliyoyapata baada ya kupata nafasi ya kipekee kabisa ya kufanya kazi na kampuni hizo kubwa duniani.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Vanessa Mdee alifunguka haya kuhusu deal hilo jipya:

Kama ilivyo ada tunaanza kwa kumshukuru Mungu kwa baraka zake na kibali chake cha kutufikisha siku njema ya leo . Nimeona nitumie fursa hii wapendwa mashabiki zangu mwanzoni mwa mwaka huu nilipitia changamoto nyingi sana, lakini kwa neema za Mungu nilitoka mahali pale na sio kuona baraka tu bali na maajabu mengi yaliyotokea kwenye maisha yangu. Ikiwemo kuwa mmoja wa familia ya Universal music group in a unique signing joint between #Universalmusicgermany #airforce1 #Universalmusicgroup”.

Vanessa hakuishia hapo aliendelea kufunguka kuhusiana na deal hilo litakalotengeneza historia.

 

Na hii ni mara ya kwanza kwa msanii wa Afrika kupata dili la aina hii yenye mkwanja mrefu sanaaaa. Hii ni habari njema kwa mashabiki zangu na ndio kwanza tumeanza mambo  makubwa zaidi yanakuja. Kumbuka kila mwisho wa Jumapili ndio mwanzo wa Jumatatu usiogope kuanza upya”.

Mwaka huu unaisha vizuri kwa Vanessa kwani amepata dili lenye pesa ndefu lakini kwenye maisha yake binafsi pia yamendaa vizuri kwani amerudiana na mpenzi wake Jux hivyo tunamtakia kila la Kheri na la Shari limuepuke.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.