Vanessa Mdee Ampongeza Mpenzi Wake Jux Baada Ya Kulamba Dili Nono

Mwanamuziki wa Bongo fleva Vanessa Mdee ‘Vee Money’ anayefanya vizuri na kibao chake cha ‘Wet’ amempa pongezi mpenzi wake na Msanii mwenzake Juma Jux baada ya kulamba Dili nono huko China.

Siku ya jana kupitia mtandao wa Instagram Vanessa na Jux walionekana pamoja wakiwa nchini China ambapo baadae Jux aliweka wazi kuwa ameenda nchini humo kwa ajili ya biashara.

download latest music    

Jux alitangaza amepata Dili nono na kampuni ya Vendome ya nchini China Kupitia bidhaa zake na Brand yake ya Africanboy ambapo kampuni hiyo itauza bidhaa zake dunia nzima.

Jux alionekana akitia Saini mkataba huo ambao unasemekana kuwa na thamani kubwa tu na moja kati ya watu aliokuwa nao pale ni mpenzi wake Vanessa.

Ambapo kupitia ukurasa wake wa Instagram Vanessa alimuandikia ujumbe huu Jux wa kumpa pongezi baada ya kufunga Dili hilo:

Tunaishi kwenye dunia ambayo kila kitu kinawezekana, hongera sana sana sana babe umepambana umeweza kuojenga African boy pamoja na Watanzania wote walioweza kukusapoti kwa Brand yako ya kijanja sasa ni muda wa kutengeneza pesa, Mungu Akubariki zaidi tuipeleke African Boy duniani # nakuona mbali bebi we piga kazi”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.