Vanessa Mdee na Jux Watangaza Tour Ya Pamoja

Staa wa Muziki wa Bongo fleva Vanessa Mdee ametangaza ujio wa tour ya pamoja na mpenzi wake Juma Jux.

Tour yao ya muziki nchini Tanzania wameipa jina la ‘In Love & Money Tour’ ambapo wapenzi hao watazunguuka mikoa minne Tanzania bara.

download latest music    

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam kwenye uzinduzi wa Tour hiyo, Vanessa Mdee amesema huu ni wakati muafaka kwa mashabiki wake na Jux kuwaunga mkono kwani tangu waanze mahusiano yao hawajawahi kupanda jukwaa moja nakuimba.

Lakini pia Vanessa na Jux wamethibitisha ujio wa Tour hiyo kwa kuweka Kwenye mitandao ya kijamii:

Jux na Vanessa wamefunguka kuwa tour hiyo itafanyika Kwenye mikoa mitano nchini ambayo ni Dar es Salaam, Mwanza, Dodoma, Mtwara na Arusha.

Lakini pia wameweka wazi kuwa Tour hiyo itarushawa Kupitia stesheni ya televisheni ya Clouds Tv kupitia Clouds Plus.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.