Vanessa Mdee: Sina Mpango wa Kuolewa Kwa Sasa Wala Kuwa na Mtoto

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri hivi sasa na albamu yake ya ‘Money Mondays’ Vanessa Mdee amefunguka na kuzima tetesi zote zilizo kuwa zinasambaa kuwa yeye ni mjamzito.

Kwa wiki chache sasa kumekuwa na tetesi kuwa Vanessa Mdee na mpenzi wake Jux wanategemea kupata mtoto wao wa kwanza hii ni baada ya picha ya Vanessa kusambaa mtandaoni ikimuonyesha akiwa na kitumbo ndii.

download latest music    

Vanessa amefunguka hayo kwenye mahojiano aliyofanya na Millard Ayo ambapo amefunguka na kuweka wazi kuwa hana mpango wa kuolewa kwa sasa wala kupata mtoto kwani kuna mambo mengi anayohitaji kufanya kabla hajafika hatua hizo.

Kwenye Interview aliyofanya na Millard Ayo ‘On air with Millard Ayo’ Vanessa aliulizwa endapo ana mpango wa kuolewa na kuzaa hivi karibuni na alifunguka kama ifuatavyo;

Kwanza unajua watu wananiuliza old are you? I am going to be 30 this year yah naingiza miaka thealathini kwaiyo nimesonga kiumri lakini naona bado kidogo lakini hiyo ni mipango ya Mwenyezi Mungu kwaiyo sijui nini kitatokea lakini kwa sasa kuna vitu vingi natamani kutimiza kabla ya kuzaa au kuolewa, natamani kuona wadogo zangu Brian na Mimi Mars wakifanya vizuri sana, natamani kushinda tuzo ya Grammy, natamani kuwa msanii mkubwa sana duniani yaani kuna kazi ambazo nazikamilisha za Universal na kwa sababu ya mipango yetu ya Universal siwezi kuwa na mtoto kwa sasa naona sio wakati sahihi kwa mimi kufanya hivyo”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.