Viongozi wa Dini Wamfanyia Dua Ommy Dimpoz.

Viongozi wa dimi ya kiislamu kutoa katika mkowa Tabora ambapo ndipo baba yake mzazi na Ommy Dimpoz anapoishi kwa sasa wamejitokeza nyumbani kwa baba mzazi huyo na kufanya dua kwa ajili ya kuombea hali ya mtoto wake ambae mpaka sasa bado yuko Afrika ya Kusini akipatiwa matibabu.

Baba mzazi wa Ommy Dimpoz aliwahi kusikika baada ya kutangazwa sana kuwa mtoto wake amekuwa mgonjwa kwa takribani miezi mitatu sasa na kusema kuwa amekuwa akitamani ana kumuona mtoto wake huyo ambae anasikia tu kwamba ni mgonjwa.

download latest music    

Ommy Dimpoz aliripotiwa kuwa amefanyiwa upasuaji ya koo na yeye mwenyewe kuthibitisha hilo huku sababu kubwa ya ugonjwa wake ikisemwa kuwa ni sumu aliwahi kunywa katika kinywaji bila yeye kujua swala hilo.

Hata hivyo Ommy alithibitihsa kuwa kwa sasa anaendelea vizuri na afya yake ingawa bado anahitaji kuwa akiripoti hospitali mara kwa mara kwa ajili ya uchunguzi wa hali yake.

Baada ya kupata ubuyu huo waandishi wa habari wa GPL waliamua kumtafuta baba mzazi wa Ommy ili kuthibitisha hilo na ndipo aliwajibu”namuombea sana mwanangu na wale waliompa sumu mwaka huu usiishe kabla Mungu hajafanya kitu kwao, naumia sana na hali ya mwanangu na ninatamani huo ugonjwa uwarudie wenyewe”

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.