Diamond Kaingizwa Matatani na Wimbo Wake Mwenyewe (video)

Mwanamuziki wa bongo fleva, Diamond Platnumz anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘Halelujah’ amejikuta katika wakati mgumu baada ya vingozi wa dini kumjia juu kutokana na nyimbo yake hiyo ya ‘Halelujah’.

Suala la dini ni moja kati ya vitu nyeti sana kwa binadamu hasa kwasababu linahusisha suala zima la imani, Mwanamuziki Diamond anajulikana kuwa ni muumini wa dini ya kiislamu, mara baada ya kutoa wimbo ambao una jina lake linasindikizwa na imani ya kikikristo (haleluya) liliibua hisia za waislamu wenzake.

download latest music    

Mwanzoni mwa wiki hii kumekuwa na video imbayo imesambaa ambayo inamuonesha Shekhe yupo msikitini akielezea kuwa hajafurahishwa na kitendo cha Diamond kuimba haleluya huku akijua ni kinyume na maadili ya dini yao lakini pia alifunguka kuwa hajafurahishwa na kitendo cha kumuona Diamond akiwa amevaa msalaba katika video ya wimbo huo na wakati ni kinyume na maadili ya dini ya kiislamu.

Tazama Video hizi Ustadhi akifunguka;

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.