“Wanawake Tuache Majungu na Wivu Tusapotiane”- Tunda

Socialite na video vixen maarufu Tunda Sebastian amefunguka na kuwasihi wanawake wapendane na wapeane sapoti badala Kupikiana majungu na kuoneana wivu.

Tunda alijipatia umaarufu zaidi wiki chache zilizopita baada ya taarifa kutoka kimapenzi na Diamond Platnumz kuenea Kwenye mitandao ya kijamii na baadae video na picha za kimahaba akiwa na mume wa mtu mfanyabiashara Kinje kuenea mtandaoni pia.

download latest music    

Ikiwa jana ilikuwa ni siku ya kusheherekea siku ya Wanawake duniani Tunda amewapa ujumbe huo mzito wanawake Akiwasihi washike upendo na waachane na chuki kwa kushikiliana na kupeana sapoti ya hali ya juu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Tunda aliandika ujumbe huu:

Women today we need to be supporting each other to set an example for the next generation….Sio mawili tu na majungu bila mwisho… Happy Women’s day”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.