Wanigeria Wamtolea Hamisa Mobetto Povu Zito Baada ya Kusema Yeye Mzuri Kuliko Wao

Mwanamitindo na muigizaji maarufu Bongo Hamisa Mobetto ambaye pia ni mama mtoto wa mwanamuziki Diamond Platnumz, ametolewa povu zito na Wanigeria baada ya kudai kuwa yeye ndio msichana mrembo Nigeria.

Wikiendi hii Hamisa alisafiri kwenda nchini Nigeria ambako aliweka wazi kuwa ameenda kufanya kazi za mitindo na designer Mkubwa nchini humo. Ambapo Hamisa aliandika kuwa amealikwa na mbunifu huyo wa mavazi kwaajili ya kupiga picha na kumtangazia mavazi yake.

download latest music    

Kupitia ukurasa wake wa Snapchat Hamisa aliweka picha yake ambayo alikuwa anarembwa na time yake lakini maneno yaliyosindikiza picha ndio yaliyozua utata na kusababisha Wanigeria kumjia juu na kumpa kichambo cha haja.

Hamisa aliandika maneno haya;

The Most Beautiful girl in Nigeria is Tanzanian”.

Baada ya kuandika maneno hayo yaliyomaanisga kuwa msichana mzuri nchini Nigeria ni msichana wa Kitanzania, hapo ndipo mtandao wa udaku mtandaoni wa nchini Nigeria unaoitwa Instablog9ja, ulizinyaka habari hizo na kuzirusha kwenye ukurasa wao wa Instagram jambo lililozua tafrani kwani Wanigeria wamemchamba Hamisa hadi akaweka ukurasa wake wa Instagram private.

Wanigeria walieleza kuwa wamekerwa na Hamisa kwenda nchini kwao na kuanza kuwadharau wanawake wa nchi hiyo na kujiona kuwa yeye ndio msichana mzuri wakati kuna wasichana wengi ambao ni Wanigeria.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.