“Wasafi Festival ni Tamasha Kubwa Halijawahi Tokea Tanzania”-Afande Sele

Msanii mkongwe wa Muziki wa Bongo fleva nchini Afanse Sele ameibuka na kuweka wazi kuwa hivi sasa hakuna msanii mkubwa Kama alivyokuwa Diamond na hivyo tamasha lake la Wasafi Festival ndio litafunika.

Suala hili limekuja kutokana na sakata linaloendelea kupamba moto hivi sasa la mabishano ya Nani zaidi kati ya Wasafi Festival na Tamasha la Clouds la Fiesta.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo kimoja cha habari, Afande Sele ameibuka na kusema hivi sasa Tamasha kubwa sana Tanzania ni Wasafi Festival na halina mpinzani kumaanisha Fiesta linakalishwa na Wasafi.

Unajua hivi sasa Wasafi ndio Real Madrid ya Tanzania ndio tamasha bora  na linaonekana kuja kuwa kubwa kuliko yote kwaiyo kushiriki katika tamasha la Wasafi ni fahari na pia naunga mkono juhudi za wadogo zetu ambao wameamua kukata minyororo ya watu waliokuwa wanatufanya watumwa na kutunyanyasa kwaiyo Wasafi ndio mapinduzi ya burudani kwanza inaongozwa na wasanii wenyewe”.

Lakini pia Afande Sele amewatolea Povu zito Clouds Fm na kuwatolea tuhuma za kutumia nguvu zao na cheo chao kuwanyanyasa wasanii na kuwataka wafanye vile wanavyotaka wao.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.