Wasanii Wahaswa Kuwa Makini Katika Kusaini Mikataba ya Kazi
Wakili wa kampuni ya Selta Tanzania Noeli Chikwindo amfanya mazungumzo na wasanii mbalimbali nchini na kuwashauri kuwa makini sana wanapokuwa wanasaini mikataba ya kufanya kazi na kampuni au menejiment mbalimbali kwa sababu wanapozingatia sheria ndipo wanapoweza kujitetea na kulinda haki zao.
Wakili huyo anasema kuwa katika mikataba ya kazi za wasanii kuna sheria kama saba ambazo wanatakiwa kuzifuata kabla ya kusaini mkabata wowote ule na wanapaswa kuzijua na kuzifatilia kila mara.
ni vema kbala ya kuweka sahihi katika mkataba ni bora kujua ni kitu gani kwanza unakuwa unasaini,lakini pia uangalia lugha inayotumika katika mikataba iyo na kama unaielewa kuepuka matatizo yanayweza kujitokeza.
Wakili huyo anasema kuwa wasanii ni kazima watambue haki zao kwanza na ndipo watambue kuwa wanaweza kufanya kazi na watu wengine hii itasaidia sana kuepuka wasanii kuwa wanalalamika kuwa wanaonewa au kuutapeliwa.