Wasanii Wamekosa Akili ya Biashara;-Ruby

Mwanadada Ruby amefunguka na kusema kuwa kukaa kwake kimya hakukumaanisha kuwa alikuwa amefulia lakini pia alikuwa akijipanga jinsi ya kuja kurudi katika soko lake na sio kwamba angeiga kile walichokuwa wakifanya wengine.

Ruby anasema kuwa wasaii wengi hawana ile akili ya biashara na muziki wamekuwa wakifanya vitu kwa kuiga tu lakini kwake ni tofauti.

download latest music    

Nilikaa kimya ili kuutengeneza muziki wangu kwanza.wasanii wengi wamekosa ile akili ya baishara na kujua kwamba muziki sio vile watu wanavyoraka wewe uwe lakini ni vile wewe unavyoutengeneza kwa sababu kama mwenzio anauza maembe sio lazima na wewe uuze maembe unaweza kuuza kitu kingine tu au ukauza kile kwa maboresho zaidi.

Ruby ambae ametoa wimbo wake mpya unaitwa niwaze aliowashirikisha The Mafik anatoa sababu ya kuwashirkisha wasanii hawa na sio watu wengine akisema,

Niliwachagua the mafik kwa sababu ni wanaume wenye sauti za kupangilia na zinaweza kukaa kwenye muziki na kufanya muziki usikike vizuri.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.