Wasanii Wanamuogopa Dudu Baya Kumsaidia Mtoto Wake
Mtoto wa msanii Dudubaya amefunguka na kusema kuwa wasanii wengi wamekuwa wakitaka kumsaidia lakini wanakuwa wanaogopa kutokana na ukorofi wa baba yake mzazi kwa wasanii wenzake.
Mtoto huyo ambae amekuwa akionekana mitaa ya Coco Beach akifanya kazi anasema kuwa wasanii tofauti kama madee pamoja na Dully sykes wamekuwa wanataka kumsaidia lakini wanakuwa kama wana uoga ambao hata yeye anauona kutoka kwao kutokana na ukorofi wa baba yake.
Hapo nyuma iliwahi kuzka tetesi kuwa mtoto huyo amekataa shule na kutaka kujiingiza katika muziki ambapo dudu baya mwenyewe alitokwa na povu zito na kusema kuwa ameshindwa kumlea mtoto huyo kutokana na ujinga anaokuwa anauonyesha wa kukataa kusoma na kutaka kuimba muziki.