Wasanii Waungana Kumsaidia Mtoto wa Muna
Mtoto wa msanii na muandaaji wa matamasha Muna love anejulikana kama Patric ambae mara ya kwanza alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya miguu na kumfanya mama ake kupitia katika majaribu yaliyomfanya muna kokoka na kumrudia Mungu ameanza kuumwa tena na kuonekana kuwa bado anahitraji uangalizi mkubwa wa madaktari.
Mtoto huyo amabe anaonekana kugusa mioyo ya watu wengi katika tasnia ya sanaa , alianza kuwekwa katika mitandao ya kijamii siku ya jana huku watu wengi wakiandika maneno ya masikitiko na yenye kutia faraja familia ya muna na ndugu zake kwa ujumla.
Hata hivyo wasanii wengi wameonekena kuguswa na tatizo hilo na kuamua kufanya harambee katika kitandao ya kijamii kupitia kurasa zao kwa ajili ya kuwaomba wadau na mshabiki kuchangia ili mtoto huyo aweze kusaidika katika matibabu yake.