Wasanii Wengi Wanaoa Ili Kutafuta Kiki- TID

Msanii mkongwe wa Bongo fleva TID amewatolea povu zito wasanii wenzake wanaotangaza ndoa na kuoa ili mradi tu watengeneza kiki kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari.

Siku za hivi karibuni Kumekuwa na trend ya wasanii wengi wa kiume kuoa hasa nje ya nchi kwa wasanii kama AY ambaye ameoa Rwanda na Ali Kiba ameoa Kenya, TID amedai hawana lolote zaidi ya kutafuta kiki.

download latest music    

Lakini pia TID amewatolea uvivu wasanii ambao wamekuwa wakitangaza kuwa wanataka kuoa lakini kiuhalisia hamna kitu mpaka leo hawajao zaidi walipata kiki za bure na katika hilo TID hakusita kumtaja swahiba wake Q chief ambaye alishawahi kutangaza ndoa siku za nyuma.

TID amefunguka hayo Kwenye mahojiano na kipindi cha Enews ya  EATV baada ya kupita takribani siku 24 tokea msanii huyo kutangaza wazi kuwa yupo katika mahusiano na mwanadada mmoja ambae alikuwa nae nchini Germany jambo ambalo wengi wao walitarajia kuoa ndoa ikifuata katika siku za usoni.

Sijasema kama ninaoa mwezi wa sita (Juni) ila tulikuwa tunajifurahisha mimi na rafiki yangu usingizi katika ‘comment’ instagram ilikuwa utani tu sijafikilia kuwa hivyo. Unajua sasa hivi watu wanataka kutengenezea kama kiki kitendo cha kuoa, kwa hiyo mimi sio mtu kutafuta kiki kwa kutumia ndoa”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.