Wastara Adai Anawacheka Wanaotumia Maradhi Yake Kumdhihaki

Muigizaji wa Bongo movie Wastara Juma maarufu kama Wastara Sajuki amedai kuwa hivi saaa amebaki anawacheka watu ambao wanatumia afya yake kumdhihaki Kwenye mitandao ya kijamii.

Siku chache zilizopita Wastara aliposti picha iliyomuonyesha akiwa hoi mahututi hospitalini na mara moja mashabiki wakaanza kumdhihaki kuwa anataka mchango mwingine

download latest music    

Lakini mara moja Wastara alijitetea na kusema kuwa picha ile ilikuwa ya siku nyingi kipindi yuko Kwenye matibabu nchini India hivyo amebaki anawacheka tu watu waliokuwa wanamdhihaki kwani yeye ndiye anajua ukweli.

Kwenye mahojiano na Za Motomoto News, Wastara alisema kuwa, hakuna anayempangia cha kuposti na kinachomuumiza ni pale ambapo kuna watu wanachungulia akaunti yake kwa ajili ya kusubiri ataposti nini ili wamtukane.

Sikuomba kuchangiwa ili nitukanwe, ilitokea tu kwa sababu ya matatizo. Kwa kifupi, wanaonitukana kwa sababu ya afya yangu, ninamuachia Mungu, kofi la Mungu ni kali sana maana sikuomba kuumwa ili nichangiwe na baadaye nitukanwe, ni mipango ya Mungu tu na atawaadhibu wanaofanya hivyo“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.