Wastara- Kuna Muda Unafika Natamani Hata Kujinyonga Kwa Jinsi Ninavyosimangwa

Muigizqji wa Bongo movie Wastara Juma au maarufu kama Wastara Sajuki amefunguka na kudai kuna wakati unafika anakuwa anatamani hata kujinyonga kwa ajili ya masimango.

Siku mbili hizi kuna picha iliyosambaa Kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha Wastara akiwa amelala kitandani hospitali huku matibabu yakiendelea.

download latest music    

Baada ya picha hizo kusambaa mashabiki walianza kumtolea povu na kumtuhumu kuwa anapenda Michango na anajiandaa kuchangisha watu kwa mara ya tatu.

Baada Ya sakata hilo MIllard Ayo Tv walimtafuta ilikujua kama anaumwa Tena au kama ni kweli anataka Michango mingine maana ile picha aliposti yeye mwenyewe.

Baada ya kuulizwa swali hilo Wastara alieleza machungu yake kuhusu jambo hilo na hata kueleza kuwa kuna muda anatamani kujinyonga kutokana na kuchoshwa na masimango:

MImi Nipo vizuri tu wala siajaandika kitu chochote na nianendelea vizuri ila watu wenyewe wanaongea wanachojisikia kwa sababu uelewa wao ni mdogo sana kwaiyo huwezi kumpangia mtu kitu cha kusema.

Yaani kuna muda najutia kwa nini nilisema matatizo yangu kwa Watanzania ni kama kuna kitu niliwakosea au nilikosea kuomba ni kitu ambacho kinanifanya nitamani hata kujinyonga kwa masimango ninayopata”.

Tetesi za Wastara kukusanya Michango kisha anaenda kutumia pesa hizo kwa kufanya biashara zilisambaa mara ya mwisho alivyochangiwa kwenda India kwa ajili ya matibabu.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.