Wastara: Najuta Kufunga Ndoa na Mbunge

Muigizaji wa Bongo movie Wastara Juma maarufu kama Wastara Sajuki amefunguka na kusema kuwa moja kati ya vitu ambavyo anavijutia kwenye maisha yake ni kufunga ndoa na Mbunge wa jimbo la Donge, Sadifa Khamis Juma.

Wastara amesema anajutia uamuzi huo kwani hakumjua vizuri kabla ya kukubali kufunga naye ndoa amesema kwamba alikubali kufunga ndoa na mwanaume huyo pasipo kumjua ni mtu wa aina gani.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya  na Kikaangoni ya East Africa Tv, Wastara amefunguka haya kuhusu ndoa yake na Sadifa:

Najuta kuwa na mahusiano na Sadifa kwa sababu sikuwa namjua vizuri. Tulifunga ndoa baada ya kujuana kwa kipindi cha wiki moja. Alikuja kwa njia ya kunipa faraja kwa vile mimi ni yatima, pia mjane lakini pia ni mlemavu. Mtu mimi akiniambia kitu kama hicho anaweza kuiteka akili yangu kabisa,”

Wastara aliolewa na Mbunge huyo kama mke wa pili mwaka jana ambapo ndoa hiyo ilidumu kwa miezi kadhaa na baadae kuvunjika kwa kile alichodai Ahadi zake hazikutimizwa kwenye ndoa hiyo.

Lakini pia Wastara amedai kuwa sababu kubwa kuachana na mumewe Sadifa ilikuwa ni pamoja na mumewe huyo kulazimisha apewe risiti zote alizokwenda nazo kwenye matibabu kwa fedha alizochangiwa na Alikiba, Makamu wa Rais Mama Samia ili yeye akalipwe fedha zote na Bunge.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.