Wastara- Pamoja na Kupata Matibabu India Hali Yangu Bado ni Mbaya

MSanii wa filamu za Bongo Movie Wastara Juma au Maarufu Wastara Sajuki amefunguka na kuweka wazi kuwa kwa sasa hali yake ni mbaya kwani anasumbuliwa na kichwa na mgongo.

Kama utakumbuka mapema mwaka huu Wastara alichangiwa na wananchi, pamoja na Serikali kwenda nchini India kwa ajili ya matibabu ya mguu ambao ulikuwa unamsumbua kwa muda mrefu.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Wastara alisema yupo kwenye mateso makubwa ya mau­mivu ya kichwa na mgongo na tarehe ya kurudi hospitali nch­ini India imeshafika lakini ameshindwa kwenda kutokana na kukosa fedha za matibabu.

Dawa nime­maliza na muda wa kurudi hospitali umefika lakini sina fedha mpaka sasa, nimefuatilia fedha za kazi niliyofanya na Wahindi walioni­sainisha mkataba wa kuwa balozi wa simu zao lakini mpaka leo hawajanilipa cho­chote na wametoroka, nimechanganyikiwa tu hapa, namuomba Waziri Harrison Mwakyembe (Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo) anisaidie ili nipate haki yangu niweze kwenda kutibiwa“.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.