Waziri Mwakyembe Kulifungia Kazi Bifu La Diamond na Ali Kiba

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amefunguka na kuhaidi kulimaliza bifu linaloendelea kati ya wasanii wawili wakubwa wa Bongo fleva.

Dkt. Mwakyembe ameweka wazi kuwa kama Mlezi wa wasanii Tanzania ameamua kulimaliza kwa kulishughulikia bifu kati ya Diamond na Ali Kiba kwani linaonekana kutoleta picha nzuri  kwenye Muziki wa Bongo fleva.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Kampuni ya Global Publishers, Waziri Mwakyembe alisema kuwa, yeye hadhani kama kuna tofauti kubwa kati ya wasanii hao bali anaona kwamba mashabiki ndiyo wanaolikuza bifu hilo kwa sababu wanazozijua wenyewe.

Nahisi mashabiki wa hawa wasanii wawili ndiyo wanaolikuza hili bifu. Lakini pia mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari vikishaandika ndipo inaonekana kuna shida lakini kumbe siyo hivyo.

Labda niseme tu kwamba, kuna kitu naandaa na hivi karibuni mtawaona pamoja na hiyo itawafanya muamini kuwa hawana bifu kama inavyojaribu kukuzwa”.

Diamond na Kiba kwa muda mrefu wamekuwa wakitajwa kuwa kwenye bifu kubwa ambapo mbali na mara kadhaa kurushiana maneno makali pamoja na kwamba wamekataa kuwa Kwenye bifu.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.