WCB Wadai Mamilioni Waliyowekeza Kwa Mavoko Hayajarudi Hata Robo

Msemaji wa Label ya WCB ambaye pia ni mmoja wa meneja wa Diamond Platnumz, Sallam Sk amemfungukia sakata hilo na kudai pesa ambazo Label hiyo zimewekeza kwa Rich Mavoko hazijrudi.

Wiki iliyopita msanii Rich Mavoko ambaye alikuwa chini ya Label hiyo kwa muda kidogo alitinga BASATA na kwenda kuwashitaki kwa mkataba wao wa kinyonyaji.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Sallam Sk ameweka wazi kuwa mpaka hivi sasa Rich Mavoko yupo chini ya WCB kimkataba zaidi.

Lakini pia ameweka wazi Kuwa mpaka sasa pesa ambayo wamewekeza kwa muimbaji huyo katika project zilizotoka haijarudi hata robo.

Mpaka sasa sielewi malalamiko ya Mavoko ni yapi kwa sababu ukisema sisi tunamnyonya mtu hicho kitu hakiwezekani alafu isitoshe Pesa ambayo tumewekeza kwa Rich Mavoko haijarudi hata robo”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.