WCB Wagoma Nyimbo Zao Kupigwa na Habari Zao Kuripotiwa na Baadhi Ya Media

Label au kundi linalofanya vizuri hivi sasa nchini WCB linaloongozwa na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz limetoa tamko rasmi la kuwataka baadhi ya media wasipige nyimbo zao.

Meneja wa label hiyo Babu Tale ametoa tamko hilo jana wakati akichonga na waandishi wa habari Kwenye uzinduzi wa Wasafi Tv Kwenye king’amuzi cha Startimes.

download latest music    

Babu Tale amevitaka vyombo vilivyokataa kupiga nyimbo zao Mwanzoni viendelee hivyo hivyo na hata visijaribu kuripoti taarifa zao.

Tunaendelea kuwaomba waendelee kushinikiza wafanyakazi wao wasipige nyimbo zetu.

Hatutaki kuona wanapiga nyimbo zetu wala kutoa habari zetu kwa sababu wao walitukataa mwanzo, tunawakataa kwa sababu wao walitukataa“.

Diamond amekuwa katika mgogoro mzito na Media mbali mbali ambazo zimekuwa hazipigi kabisa nyimbo zake ambazo ni Clouds Media na hata East Africa Radio na Tv.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.